Friday, May 19, 2017




 Makipa wa Kenya, Ian Otieno (Kushoto) na Boniface Oliech (Kushoto) wakiwa mazoezini

Kocha wa timu ya taifa ya soka nchini Kenya, Stanley Okumbi amewaita wachezaji 26 kambini kwa minajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Angola tarehe 4 mwezi ujao.
Mchuano huo wa kimataifa utapepetwa mjini Machakos mashariki mwa taifa hilo huku mechi hiyo ikitumika kuiandaa Kenya kabla ya kombe la CHAN mwaka ujao.
Hata hivyo kikosi hicho kimewajumuisha wachezaji wanaocheza soka ya kulipwa nyumbani pekee. Wataripoti kambini mapema wiki ijayo kwa maandalizi zaidi.

0 comments:

Post a Comment