
walioketi ni Wasimamizi wa Kamati ya Olimpiki
nchini Kenya.
Wasimamizi wa Kamati ya Olimpiki
nchini Kenya, NOCK, wameshtakiwa kwa njama za wizi na usimamizi mbaya wa
fedha na sare za kikosi cha Kenya katika mashindano ya Olimpiki
yaliyofanyika mjini Rio , Brazil mwaka uliopita.
Ofisi ya
Mkurugenzi wa mashtaka nchini Kenya, ODPP imetangaza kuwa, baada ya
kutathmini uchunguzi, maafisa hao wanastahili kushtakiwa kwa makosa
hayo. Wasimamizi hao wakiwemo msimamizi wa timu ya Kenya kwenye Olimpiki, Stephen Soi, aliyekuwa naibu mkuu wa ujumbe wa Olimpiki, Bernard Ekumbo, katibu mkuu, FK Paul na naibu meneja wa timu hiyo, Pius Ochieng watafikishwa mahakamani baadaye mwezi huu kujua hatma yao
0 comments:
Post a Comment