Friday, May 19, 2017


XAVI-AL SADDXavi, Mkongwe aliechezea Barcelona kwa Miaka 17 na kuhamia Al Sadd ya Qatar Mwaka 2015, anahisi Real Madrid itatwaa Ubingwa wa La Liga Jumapili lakini anaona Juventus ya Italy itaibwaga Real kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI hapo Juni 3.
Jumatano iliyopita Real, chini ya Kocha Zinedine Zidane, iliitandika Celta Vigo 4-1 na kuongoza La Liga Pointi 3 mbele ya Barcelona huku kila Timu ikibakiza Mechi 1 tu itakayochezwa Jumapili.
Hiyo Jumapili Real wanahitaji Pointi 1 tu Ugenini na Malaga ili kuzoa Ubingwa wao wa kwanza wa La Liga tangu 2012 lakini Barca wataombea yatokee yale ya Msimu wa 1991/92 wakati Tenerife ilipoifunga Real na Ubingwa kupeperuka kwenda Barca katika Mechi ya Mwisho ya Msimu.
Lakini Xavi, alietwaa Mataji 8 ya La Liga akiwa na Barca, amekubali kuwa safari hii Real hawawezi kuteleza.LALIGA-MEI20
Ameeleza: “Ni ngumu La Liga kuiponyoka Real. Wao ni Timu imara. Wana Kiungo imara kina Toni Kroos, Luka Modric, Isco…..nawapenda wote!”
Aliongeza: “Malaga wapo vizuri na kuwafunga kwao ni ngumu. Wanapaswa kuleta miujiza kama ya Tenerife ili Barca watwae La Liga. Vipigo kwa Barca Nyumbani na Alaves na Deportivo La Coruna Ugenini vimeleta balaa kwa Barca Msimu huu!”
Wakitwaa La Liga, Real watakuwa njiani kutwaa Dabo kwani wapo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI watakayocheza na Juventus hapo Juni 3 huko Cardiff, Wales wakiwania kuwa Klabu ya Kwanza kutetea vyema Ubingwa huu.
Lakini Xavi anaamini Fainali hiyo ni ngumu mno na anaombea Kipa Mkongwe wa Juve, Gianluigi Buffon, atamaliza subira yake ya muda mrefu ya kutotwaa Kombe hili.
Xavi ameeleza: “Juventus ni wazuri sana. Wameonyesha hilo kwa kuwatupa nje Barca na pia wana ngome imara. Hii Fainali ni 50-50. Nilimsikia Buffon akisema hajatwaa Kombe hili. Anastahili kulibeba pamoja na Ballon d'Or!”.
LA LIGA 
Ratiba:
Raundi ya 38 – Mechi za Mwisho
Ijumaa Mei 19
21:45 Granada v Espanyol 
Jumamosi Mei 20
18:00 Deportivo v Las Palmas 
18:00 Sporting Gijon v Real Betis 
18:00 Leganes v Alaves 
Jumapili Mei 21
17:45 Atletico Madrid v Athletic Club 
17:45 Celta Vigo v Real Sociedad 
17:45 Sevilla v Osasuna 
17:45 Valencia v Villarreal 
21:00 Barcelona v Eibar 
21:00 Malaga v Real Madrid

0 comments:

Post a Comment