Friday, May 19, 2017

 


TOTAL AFCON U17 GABON2017>NUSU FAINALI, FAINALI KOMBE LA DUNIA HIZOOO!
MARA baada ya Serengeti Boys kuichapa Angola 2-1 hapo Jana huko Stade de L’Amitle, Mjini Libreville Nchini Gabon, kwenye Mechi ya Kundi B la Mashindano ya TOTAL U-17 AFCON GABON 2017, ikafuatia Mechi nyingine ya Kundi hilo na Mabingwa Watetezi Mali kuipiga Niger 2-1.
Awali Jana Tanzania, maarufu kama Serengeti Boys, iliibwaga Angola 2-1 ikiwa ni Mechi yao ya Pili ya Kundi B baada kuanza kwa Sare ya 0-0 na Maabingwa Watetezi Mali.
Matokeo ya Mechi 2 za kwanza za Kundi B zimeziweka Serengeti Boys na Mali juu kileleni zote zikiwa na Pointi 4 kila moja zikifuatia Niger na Angola zenye Pointi 1 kila moja.
Hii inamaanisha, ili kutinga Nusu Fainali ya Mashindano na hivyo pia kufuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia za U-17 huko India Mwezi Oktoba, Serengeti Boys wanahitaji Sare tu kwenye Mechi yao ya mwisho na Niger.
++++++++++++++++++++++

Toka Kundi A, Timu hatari ya Ghana tayari ishatinga Nusu Fainali, na hivyo pia kwenda India, huku ikiwa na Mechi 1 mkononi.
Serengeti Boys watamaliza Mechi zao za Kundi B hapo Jumapili Mei 21 kwa kucheza na Niger huko Stade de POG, Port Gentil.
TOTAL U-17 AFCON GABON 2017
MSIMAMO:
AFCON-U17-TEBO-2MATCHES
Ratiba/Matokeo:
**Saa za Bongo
***KUNDI A Mechi kuchezwa Mjini Port Gentil KUNDI B Mjini Libreville
MAKUNDI:
Jumapili Mei 14
KUNDI A
Gabon 1 Guinea 5
Cameroun 0 Ghana 4
Jumatatu Mei 15
KUNDI B
Mali 0 Tanzania 0
Angola 2 Niger 2
Jumatano Mei 17
KUNDI A
Guinea 1 Cameroun 1
Ghana 5 Gabon 0
Alhamisi Mei 18
KUNDI B
Tanzania 2 Angola 1
Niger 1 Mali 2
MECHI ZA MWISHO ZA MAKUNDI
Jumamosi Mei 20
KUNDI A
2030 Gabon v Cameroun [Stade de POG, Port Gentil]
2030 Guinea v Ghana [Stade de L’Amitle, Libreville]
Jumapili Mei 21
KUNDI B
2030 Mali v Angola [Stade de L’Amitle, Libreville]
2030 Tanzania v Niger [Stade de POG, Port Gentil]
NUSU FAINALI:
Jumatano Mei 24
Stade de POG, Port Gentil
1730 Mshindi Kundi A v Mshindi wa Pili Kundi B
Stade de L’Amitle, Libreville
2030 Mshindi Kundi B v Mshindi wa Pili Kundi A
Jumapili Mei 28
Stade de L’Amitle, Libreville
1730 KUGOMBEA MSHINDI WA 3
2030 FAINALI

0 comments:

Post a Comment